Jumanne, 31 Desemba 2013

Dodoma ni Historia hii haijawahi Kutokea

Mcheza kwa hutunzwa na Mtu kwao waswahili wanasema hivyo yule super nyota wa Dodoma mwaka huu 2013 JacoBeat anafunga mwaka kwa staili ya tofauti haija wahi kutokea hiyo mkoani Dodoma
  Akizungumza na waandishi wa habari Jacobeat amesema
",Baada yakumaliza video ya ayayah sasa tunamaliza mwaka kwa burudani yakutosha siku ya mkesha wa mwaka mpya tutapiga show mbili ndani ya usiku mmoja tukianza na viwanja vya kidongo nakumalizia show ya nguvu huku tukizindua video kwa mara ya kwanza pale club laaziz na kama haitoshi alhamisi pale maisha club dodoma video itatambulishwa pia kumaliza kiu yako tuungane katika sehemu nilizokutajia kwa burudani ya nguvu"
moja kati ya vipande vya video mpya itakayofanyiwa uzinduzi
    • Korumba Victor Moshi
  1. December 29 via mobile
    hello fanz,Baada yakumaliza video ya ayayah sasa tunamaliza mwaka kwa burudani yakutosha siku ya mkesha wa mwaka mpya tutapiga show mbili ndani ya usiku mmoja tukianza na viwanja vya kidongo nakumalizia show ya nguvu huku tukizindua video kwa mara ya kwanza pale club laaziz na kama haitoshi alhamisi pale maisha club dodoma video itatambulishwa pia kumaliza kiu yako tuungane katika sehemu nilizokutajia kwa burudani

    Nahichi ndicho alichokiandika mmoja wa viongozi juu ya Wise one Ambae nae atakuwepo kwenye show hiyo pamoja na Jacobeat

  2. Hii ndo zawadi yangu binafsi kwa Msanii WIsE OnE ambaye naomba nimtambue kama msanii Bora wa kiume wa mwaka 2013.
    Ingrdients:Amefanya video mbili ndani ya huu mwaka, anafanya harakati za kupush mziki wake nje ya DODOma, hits,kama MALAIKA,KILAZA,AYA yaYAYa,KAMA NINGEJUA,My LoVE..pia ameweza kupata fursa ya kufanya showS nje ya Mkoa.
    — with Jaco Beatz and 2 others.
  3. Huu ndo Utamu wa video ya ayayah ni noma sana
Ni bonge moja la video nashow ya kueleweka hautakiwi kukosa hii
          Funga mwaka na Peremende Dodoma

Jumapili, 22 Desemba 2013

HOTUBA YA ZITTO KABWE NA MAPOKEZI YAKE - KIGOMA, JANA 21 DESEMBA 2013‏..

HOTUBA YA ZITTO KABWE NA MAPOKEZI YAKE - KIGOMA, JANA 21 DESEMBA 2013‏..

Zitto Kabwe akihutubia wananchi wa Kigoma jana.
Wananchi wakiwa na mabango ya kumpokea Zitto.
HOTUBA YA MH ZITTO Z. KABWE - KIGOMA – 21 DESEMBA 2013
Leo nina furaha kubwa sana kwani baada ya safari ndefu na yenye changamoto nimerudi nyumbani kuwasalimu wananchi wenzangu! Na hii si salamu za kawaida bali nawasalimu kwa salaam za demokrasia, uadilifu, uzalendo na uwajibikaji. Nawasalimu si kama mbunge bali kama mwana wenu wa Kigoma! Na popote niendapo najivunia kujitambulisha kama Mtanzania; kama mwenyeji wa mkoa wa Kigoma na zao la Ujiji.
Tuna mengi ya kujivunia kama taifa lakini Ujiji na watu wake mna nafasi ya pekee katika historia. Watu wa Ujiji mlipokea harakati za kudai uhuru wa nchi yetu mapema kabisa mapambano ya uhuru yalipoanza. Watu wa Ujiji mlikuwa wa kwanza kabisa kupokea mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Na Jimbo la Kigoma Mjini ilikuwa miongoni mwa majimbo ya mwanzo kabisa kutoa mbunge wa CHADEMA mwaka 1995. Kabla ya hapo mlitoa madiwani wengi mwaka 1994.
Wakati Watanzania wengine wakiwa wanajiuliza mara mbili mbili kuhusu kujiunga na vyama vipya vilivyoanzishwa, watu wa Ujiji, watu wa Kigoma hamkusita kupokea mabadiliko. Wengi wamepoteza maisha yao, wengine kazi zao na wengine hata ndoa zao katika kupata mbegu ya mabadiliko katika nchi yetu. Nawataka msichoke. Wekeni nguvu mpya katika kusimika mabadiliko kwani bado kazi ya kuimarisha demokrasia katika nchi yetu haijaisha na inahitaji uvumilivu, kusameheana na kuaminiana.
Na nchi yetu Tanzania ni nchi inayoonyesha uwezo mkubwa katika kupendana, kuaminiana, kuvumiliana na hata kusameheana. Na haya si maneno tu ambayo ninayazungumza kama mwanasiasa. Hii ni hali halisi na maisha niliyoyaishi kwa mifano nilipokuwa ninakua na kusoma katika shule ya Msingi Kigoma na baadaye Shule ya Sekondari Kigoma. Malezi yangu yalikuwa yanaongozwa na jamii nzima ya Kigoma.
Nimekuwa nikiwaeleza rafiki zangu niliokutana nao kwenye masomo na kwenye siasa kwamba nimeanza kuvaa viatu kwa mara ya kwanza nikiwa darasa la tatu. Viatu hivyo viliitwa 'asante Salim' vilivyokuwa vinatengenezwa na Kampuni ya Bora Shoes. Vililinunuliwa na mama Coretha Furugunya ambaye tulikuwa tunakaa mtaa mmoja wa Kisangani Mwanga. Mama Coretha hakuninunulia viatu kwa sababu alikuwa ana uwezo mkubwa, la hasha! Alifurahishwa na matokeo yangu ya mitihani ya darasa la pili kwenda la tatu.
Ninaamini kitendo cha mama huyu ni ushahidi wa uungwana, upendo na hata uwajibikaji ambao tunao sisi watanzania. Uwajibikaji kwani alichukua jukumu kunilea ingawa hakuwa mzazi wangu, lakini aliona kuwa kama mwanajamii ana nafasi kubwa katika kuwaendeleza watoto wote. Jamii hii ya watu wa Kigoma ilinifunza kuwa nikijitahidi na kukazana kwa bidii kwenye masomo na majukumu, nitafanikiwa. Siwezi kusahau somo hili katika maisha yangu na ni somo hili ndilo limenifanya nijitahidi kwa kadiri ya uwezo wangu kuwatumikia kwa uadilifu na mafanikio ya hali ya juu sana.
Nikiwa nimejaa matumaini haya kuhusu wananchi wenzangu, leo nataka niwakumbushe kwa nini kama jamii tulichagua kufuata njia ya demokrasia. Demokrasia ina maana pale ambapo inatumika kuleta mabadiliko chanya kwenye maisha ya wananchi. Maisha yanayotakiwa ni yale yanayomwezesha mwananchi kupata huduma zake stahili kama Elimu, Afya, Maji na miundombinu. Demokrasia haina maana pale wananchi wanakufa njaa kwa kukosa ajira na kukuza umasikini.
Demokrasia inahusu maendeleo. Tumejitahidi kwa upande wetu kuondoa mkoa wa Kigoma kutoka mikoa isiyo na miundombinu kabisa ya maendeleo mpaka kuwa mkoa unaotumika kama mfano kwa miradi mingi ya Maendeleo ikiwemo Daraja la Malagarasi, Uwanja wa ndege wa Gombe-Mahale, barabara za lami na upanuzi wa Bandari, ujenzi wa bandari ndogo mpya na ujenzi wa kituo cha Usafirishaji Mwandiga.
Asije mtu akasema yeye ndio kafanya haya. Haya ni matunda ya nyinyi watu wa Kigoma kupokea demokrasia na bila woga kuchagua viongozi wenu bila kujali vyama bali kwa kuangalia uwezo. Haya ni matunda ya viongozi wenu kupaza sauti yenu kwenye baraza la Taifa, Bunge. Haya ni matunda ya uvumilivu wenu na uamuzi wenu wa kutaka maendeleo. Juhudi hizi lazima ziendelezwe kwa nguvu zote ili kuhakikisha kuwa nafasi ya mkoa wa Kigoma katika uchumi wa Tanzania inaonekana dhahiri na hivyo kuchochea maendeleo ya nchi yetu kwa kuwa kituo cha biashara katika nchi za maziwa makuu.
Lakini tukumbuke pia kuwa Demokrasia ni Uwajibikaji. Katika kipindi cha utumishi wangu kwenu,kutokana na malezi niliyoyapata kutoka kwenu,nimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa Serikali inawajibika kwa Wananchi. Nakumbuka wakati napambana kuhusu sheria mbovu ya madini kuna watu hapa nyumbani walisema 'sasa huyu kawa mbunge wa Taifa' lakini watu wengi zaidi wakasema tumemtuma Dodoma kusemea Watanzania wote na sio Kigoma tu.
Tuliweza ndani ya miaka mitano kufanya mabadiliko makubwa sana kwenye sera ya Madini na sheria ya madini ambapo baadhi ya mambo ambayo yalikuwa hayafikiriki sasa yametungiwa sheria ikiwemo Serikali kuwa na hisa kwenye migodi, Tanzanite kumilikiwa na Watanzania sio chini ya asilimia 50 na kuzuia kabisa wageni kuchimba vito vya thamani.
Uwajibikaji ulipelekea kumshinikiza Rais kufanya mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri kwa kuwafukuza mawaziri wanane mwaka jana. Hii ilitokana sio tu na hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu bali pia ushiriki mkubwa wa wananchi kupitia simu na mitandao ya kijamii ambapo wabunge walishinikizwa kuweka saini kwenye karatasi za kumtoa Waziri Mkuu.
Toka wakati huo kumekuwa na utaratibu sasa ambapo wabunge hawaoni taabu kutaka uwajibikaji waziwazi ili kuzuia ubadhirifu wa fedha za Umma. Ni hivi jana tumeshuhudia mawaziri wanne wamejiuzulu na kufukuzwa kazi kutokana na kashfa ya operesheni Tokomeza ujangili iliyoibuliwa na ripoti ya kamati ya bunge. Mabadiliko haya ni hatua muhimu katika kuimarisha demokrasia yetu.
Pamoja na matunda haya mengi mazuri lakini bado kuna changamoto katika juhudi zetu.

Changamoto kubwa tuliyonayo wananchi ni kukosekana kwa imani katika demokrasia yetu.
Kutoaminiana. Ni dhahiri kuwa kutoaminiana katika nchi yetu kumekuwa kwa kiasi kikubwa. Taarifa za kitafiti zinaonyesha kuwa katika kila Watanzania kumi, wanane hawaaminiani. Ni changamoto kubwa sana. Wananchi wameacha kutuamini wanasiasa na wanasiasa wameacha kuaminiana wenyewe kwa wenyewe.

Hivi sasa uongo umegeuzwa kuwa ukweli na ukweli umekuwa ni uongo. Hivi sasa ukitaka kuwa mwanasiasa maarufu inabidi ujue kudanganya na ukitaka kuitwa mwanasiasa msaliti inabidi uwe msema kweli. Kukosekana kwa uaminifu na kuaminiana imekuwa ni kansa katika siasa zetu. Itachukua muda mrefu sana kujenga demokrasia imara katika nchi yetu kama hatutapata jibu la changamoto hii ya kutoaminiana na kugeuza uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa uongo. Hivi sasa ukweli umekuwa unatengenezwa badala ya kutafutwa.
Ni majanga! Juzi bungeni Mwanasheria Mkuu wa Serikali alielekeza shutuma kwangu kwamba sikushirikiana na kamati maalum iliyoundwa na Bunge kufuatilia mabilioni ya uswisi na kwamba chini ya kiapo nilisema sina majina ya watu wenye akaunti huko Uswisi. Huu ulikuwa ni uongo. Ni uongo kwa sababu niliitika wito wa kamati hata nilipokuwa katika mafunzo ya mgambo huko Tanga na nilikutana nao mara nne.
Ni uongo kwa sababu niliwapa wajumbe wa Kamati Maalaum maelezo na taarifa nyingi sana kuhusu utoroshwaji wa fedha nje ya nchi na umiliki wa mali nje ya nchi kinyumecha sheria. Ni uongo kwa sababu mimi kutotaja majina haya haina maana sina majina, bali ni kwamba ninaheshimu utaratibu na nimeachia vyombo husika vikamilishe uchunguzi. Kwani mimi kama mtu binafsi nikianza kuchukua majukumu ya taasisi ninaweza kutia dosari harakati hizi muhimu na hata kupelekea mchakato mzima kuvurugika. Sitaingia mtego huu! Lakini hatua hii ya Mwanasheria Mkuu imenipelekea kujiuliza maswali mengi kwa mfano uongo kama huu ulifanywa kwa malengo gani? Na ninajikuta hata mimi ninaingia katika hali ninayoilalamikia ya KUTOAMINIANA.
Lakini mtambue pia kuwa kutoaminiana kunaleta kutovumiliana. Hivi sasa kuwa na mawazo tofauti katika vyama vya siasa au hata asasi za kijamii ni uhaini. Lakini bila kuenzi tofauti za mawazo hatuwezi kujenga vyama imara wala Taifa imara. Demokrasia imara ni zao la tofauti za mawazo na uhuru wa mawazo.
Kama hatuwezi kujenga vyama vinavyorutubisha uhuru wa mawazo na tofauti za mawazo, tutajenga Taifa lenye watu wenye kuogopa na waliojaa woga. Wanachama wanapoogopa uongozi ni udikteta, lakini uongozi unapoogopa wanachama ni demokrasia. Bila demokrasia ya uwazi na kuvumiliana tutakuwa Taifa la kidikteta. Lazima vyama vya siasa, viongozwe kwa namna ile ile ambayo Taifa litaongozwa.
Demokrasia bila kuaminiana, demokrasia bila kuvumiliana sio demokrasia ya kweli.
Juzi nilipoingia Bungeni kwa mara ya kwanza baada ya matukio kadhaa yanayoendelea ndani ya chama chetu nilikaa pamoja na mbunge Tundu Lissu. Wabunge wengine walidhani tutarushiana ngumi na badala yake ikawa ni vicheko na mazungumzo. Hii ni kwa sababu sina chuki na mtu yeyote yule.

Mmenifunza kutojenga chuki na watu na badala yake kuchukua kila tukio kama changamoto ya maisha. Siasa ni kupambanisha mawazo tofauti na hatimaye kutafuta suluhu ya pamoja. Na siasa ina misingi yake ambayo sisi wanasiasa huwa tunasahau kwa maksudi. Msingi wa siasa ni kuwa inapaswa kuleta unafuu wa maisha ya wananchi na sio malumbano tu ya kurushiana maneno na kuzushiana ili kujijengea umaarufu wa kisiasa. Siasa si kuwekeana chuki na kuonyeshana ubabe.
Na hapo ni muhimu muelewa wanaKigoma mnapoambiwa kuwa eti ninapofuatilia mabilioni ya Uswisi ninatafuta umaarufu, ni uongo! Mnaposikia eti kukataa kwangu kuchukua posho ni unafiki na kujitafutia umaarufu, ni uongo! Kinachonisukuma kufanya vyote hivi ni ninyi. Ninasukuwa kila ninapowaona watoto bado wanatembea bila viatu;kila ninapoona akina mama wanapoteza maisha yao katika uzazi;kila ninapoona vijana ambao hawana uhakika wa kupata hata mlo moja kwa siku kwa kukosa kazi; ninapoona wazee wa Kigoma kukosa hata shilingi mia moja kununua chai asubuhi.
Ninawaona si wanaKigoma bali mamilioni ya watanzania wakiishi katika hali hii. Alafu nalinganisha na taarifa tunazozipata kuhusu ufujaji na utoroshwaji wa pesa zetu. Hebu sasa linganisheni na ukweli kuwa ripoti ya kimataifa iliyotolewa hivi karibuni imeonyesha kuwa mwaka 2010 pekee, jumla ya dola za kimarekani milioni 1315 (bilioni 1.3), yaani shilingi trilioni  2,113,930,000,000 (sh trilioni 2.1) zilitoroshwa kutoka nchini Tanzania. Mwaka 2011 kiasi cha dola za kimarekani milioni 817 yani shilingi za kitanzania zipatazo trilioni 1,315,370,000,000 (trilioni 1.3) zilitoroshwa.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa jumla ya fedha za Watanzania zilizotoroshwa nje ya nchi katika miaka kumi iliyopita zilifikia dola za kimarekani milioni 4526 (bilioni 4.5) sawa na shilingi za kitanzania trilioni 7,286,860,000,000 (trilioni 7.3).  Nimewatajia hapa namba chungu nzima na matrilioni na mabilioni hayaleti maana. Lakini hii ina maana kwamba kiasi cha pesa zilizotoroshwa katika miaka 10 pesa - robo yake tuingeweza kujenga barabara ya lami ya kiwango cha juu kabisa kutoka Kigoma mpaka Dar-es-salaam! Pesa hizi zingeweza kuajiri na kuwalipa vizuri walimu, madaktari na wafanyakazi wengine ili kuhakikisha tunapata huduma bora na kutengeneza ajira bora kwa vijana wetu.
Pesa hizi zingeweza kununua madawa muhimu na kuokoa maisha ya maelfu ya akina mama tunaowapoteza kila mwaka wakati wa uzazi. Pesa hizi zingeweza kuwanunulia watanzania wote si watoto tu angalau pea 10 ya viatu. Sasa nikitafakari haya siwezi kuchapa usingizi mnono na kufumbia macho utoroshwaji wa fedha au matumizi mabaya ya fedha za umma kwa njia ya sisi wabunge kujilipia posho! Hapana! Nafsi yangu hainiruhusu kukaa kimya kwa kuogopa kuitwa mbinafsi au msaliti!
Lakini naomba niwasihi kuwa katika nyakati kama hizi za changamoto za kisiasa jambo la msingi kuliko yote ni kutulia maana hakuna linalotokea bila sababu. Licha ya kwamba kuna watu wengi wanapaza sauti zao katika mambo haya lakini pia kuna wengi zaidi ambao wapo kimya lakini wana mawazo yao, ndani na nje ya chama chetu;ndani na nje ya Serikali na ndani nanje ya nchi yetu. Ndio maana lazima kuibadili nchi yetu ili kuweza kuhakikisha kila raia anakuwa na fursa ya kutoa mawazo na fikra zake zinakuwa huru.
Maisha ni mabadiliko; mabadiliko hayana ukomo; mabadiliko hayazuiliki kwa sababu bila mabadiliko hakuna ukuaji, bila mabadiliko hakuna maendeleo. Mabadiliko ni kiu kikubwa cha Tanzania kwa sababu mabadiliko huleta matumaini. Na kiu hii ni kubwa zaidi kwetu sisi vijana wa kizazi hiki kipya. Siasa za kizazi kipya cha viongozi ni siasa za majawabu ya kero za wananchi. Siasa za mabadiliko ni siasa za kujenga na kuimarisha; ni siasa za kuaminiana na kuheshimiana hata pale mnapopingana kimawazo. Ninataka tujenge siasa mpya Tanzania;siasa za mabadiliko; siasa zinazojenga matumaini ya kweli;siasa zinazowajali na kuwajengea uwezo wananchi wa Tanzania. Mungu ibariki Tanzania.

Jumamosi, 21 Desemba 2013

SIMBA WATAKATA WACHUKUA MTANI JEMBE

SIMBA WATAKATA WACHUKUA MSHINDI JEMBE



 Wekundu wa Msimbazi simba ya jijini Dar es Salaam leo imefanikiwa kwa mara nyinge kuzima kidomo domo, mikogo na mbwe mbwe za kila namna za watani wao wa jadi Yanga kwa kuwafunga magoli 3-1 katika mchezo maalum wa NANI MTANI JEMBE mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hii leo.
 katika mchezo huo Magoli ya simba yaliwekwa kimiani na mshambuliaji wake mahiri mwenye kasi nyingi na mbinu lukuki za ufungaji Hamisi Tambwe ambaye alipachika magoli 2 huku bao la tatu likifungwa na mchezaji aliyesajiliwa dirisha dogo kutoka Mtibwa Awazi Juma huku goli la Yanga likifungwa na Emmanuel Okwi.
 Patashika ya kuwania mpira
Hali jukwaa la yanga ilikuwa si shwari sana...
Ngome hata iwaje ndio Simba walipita...
Simba wao ilikuwa shangwe tu.
CHANZO : FATHER KIDEVU



Ijumaa, 20 Desemba 2013

Leo ndo Leo bungeni Pinda kuendelea kuwa waziri mkuu au laa!

FOMU ZA KUMNG’OA PINDA ZALETWA BUNGENI

Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali.
 
Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, ameingia na fomu bungeni hivi punde kwa ajili ya kukusanya saini za wabunge za kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, baada ya ripoti iliyofichua maovu yaliyofanyika katika Operesheni Tokomeza.

Mtayarishaji Bora wa Video mkoani Dododma ataoa somo

ATTENTION PLEASE  Mtayarishaji wa Video kali mkoani Dodoma Erick Backamaza atoa somo kwa wasanini wa Dododma
hii ni kwa wahusika...
Mziki wa Dodoma upo Chini na kuna uwezekano mkubwa wa kuendelea kuwa chin licha ya mabadiliko makubwa ndani ya Mwaka huu 2013.
Wasanii ni wavivu na wazembe pia hawajitumi,wanasubiri miujiza ili watoke. Wengi wana Record BURE ndomana mziki wao hawauhurumii na hawahangahikii k2, wanaolipia kidogo wakifurukuta nyimbo inaishia media za hpa hpa mjin, Prisenters wa Media wanajarb kuplay part yao japo nao wanazingua ila wasanii hawana ukarib na watangazaji na djz kikaz bar kisela tu.
Kama mabadiliko binafsi ya mtu mmoja mmoja hayatotokea GEM itawafunga kamba DAILY.
Fanyen kaz na Tangazeni kazi zenu kwa nidham ya gemu na kipaji ulichonacho, Msilidhike na kulipwa 10000 kwene show,Fanyeni kazi mlipie mziki wenu ndipo producerz watafanya kaz nzur na prizenters wataheshim kaz zenu,na ndipo mtatangaza kaz zenu
Ni hayo tu
Kwa wasio jua huyu ndie mtayarishaji bora wa Video na Move kwa mwaka 2013 mkoani Dodoma

Jumamosi, 14 Desemba 2013

Inasikitisha South Afrika

WAKAZI wa kijiji cha Qunu ambako kiongozi wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela anatarajia kuzikwa kesho, wameelezea masikitiko yao dhidi ya taarifa kuwa hawatahudhuria maziko hayo. “Inauma sana kukosa....... http://ow.ly/rLggs

Alhamisi, 12 Desemba 2013

Rais JAKAYA KIKWETE Ang'ara South Africa

South Africa kuonyesha kuwa inatambua ubora wa Rais wetu Mheshimiwa J.K kikwate imempa nafasi naheshima ya pekee sana
Viongozi wengi wanaheshimika ndani na nje ya Ulaya,lakini kitendo cha Wana Afrika Kusini kukumpa heshima  ya kutambulisha ugeni mzito basi ni FAHARI NA HESHIMA KUBWA KWA WATANZANIA NA HUO NDIO URAFIKI MWEMA KWAO NA SISI.

AHSANTE NDUGU ZETU WANA AFRIKA KUSINI,AHSANTE JAKAYA KIKWETE.

Lema amvaa Zitto Bungeni

Mhe Godbless Lema (MB) – Arusha Mjini

Leo kaweza kunena bungeni na kusema kuwa pesa za uswis zisiwe ngonjera kila siku kuongea tu juu ya swala la pesa za uswis wakati majina yapo na Zitto kabwe anayo na anaweza kuwataja au kumpa CAG aweze kuchukua hatua ila kimya kila siku sasa kama inasindwa kutaja basi anaweza kukabizi majina hayo nikaweza kutaja kwani hayo majina akutakiwi mpaka uwe na kinga ndio uweze kutaja hayo majina kinga ni wewe mwenyewe kutaja"""Ni kauli ya Mhe Godbless Lema (MB) – Arusha Mjini leo bungeni Dodoma,
Kaongea vitu vya msingi maana toka niskie Zitto akiongelea swala la mapesa ya uswisi ni mda mrefu mpaka sasa ila amna hatua zozote kuchukuliwa,

Neno lako juu ya Swala hili. .

Jumatano, 11 Desemba 2013

ZITTO NA RUFAA YAKE

Taarifa ya leo ya mwanasheria wa Zitto Kabwe, maamuzi ya Zitto, vurugu kwa Dr. Slaa na mengine

k2Taarifa iliyotolewa leo December 11 2013 na Albert Msando ambae ni Mwanasheria wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuhusu zile headlines za hivi karibuni za kuvuliwa vyeo CHADEMA imesema ‘baada ya kupokea barua yake ya mashtaka 11 tarehe 01/12/2013 ambayo anashitakiwa nayo na iliyomtaka ajitetee kwa maandishi, Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe (MB) jana tarehe
10/12/2013 amefanya hivyo kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uendeshaji za Chama’
Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe (MB) ametoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa Chama kumueleza nia yake kukata rufaa Baraza Kuu la Chama kupinga hatua iliyochukuliwa na Kamati Kuu dhidi yake kumvua nyadhifa zake ndani ya Chama ambapo kuna sababu mbili za msingi za kukata rufaa;
1. Utaratibu wa kuchukua hatua za nidhamu ulikiukwa. 2. Sababu za kuchukuliwa hatua hizo sio sahihi.
Utaratibu ambao unatakiwa kufuatwa kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kiongozi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uendeshaji ni kama ifuatavyo;
Kanuni ya Uendeshaji inasema kiongozi yeyote hatochukuliwa hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashitaka yake kwa maandishi na mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu mashitaka kwa maandishi pia tunapenda ijulikane kwamba Kanuni ya Uendeshaji 6.5.2 (a), (b), (c) na (d) kama ilivyorekebiswa Januari 2013 inasema;
k2Kwa mujibu wa ibara ya 5.4.3 na 5.4.4 ya Katiba mwanachama yeyote hatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama kuachishwa ama kufukuzwa uanachama bila kwanza;
a) Kujulishwa makosa yake kwa maandishi na kutakiwa kutoa majibu katika muda usiopungua wiki mbili.
b) Kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.
c) Mwanachama atajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao mnamo wiki mbili baada ya kusikilizwa.
d)Kamati Kuu inaweza kuchukua hatua za dharura bila kuzingatia utaratibu (b), (c) hapo juu kama itaona maslahi ya Chama kwa ujumla yanaweza kuathiriwa isipokuwa mwanachama au kiongozi anayelalamikiwa atalazimika kuitwa kwenye kikao husika.
Naomba nichkue fursa hii kufafanua kuwa uongozi wa chama ulifanya mkutano na waandishi mnamo tarehe 26/11/2013 na kusema kwamba marekebisho haya ya Kanuni ya mwaka 2013 ambayo nimewawekea hapo juu, ndiyo utaratibu waliofuata pia walieleza kuwa sikuwa naifahamu na nilidanganywa kwani Kanuni ilishabadilishwa.
Mabadiliko haya ambayo ni katika kipengele (d) kuhusu hatua ya dharura iliyochukuliwa na Kamati Kuu haikugusa kipengele (a) cha Kanuni. Yaani ni kuwa hata kama Kamati kuu itachukua hatua ya dharura kwa mujibu wa kipengele (d), bado kipengele (a) ni lazima ifuatwe na inatamka wazi sharti la kiongozi kupewa mashtaka kwa maandishi na kupewa nafasi ya kujibu kwa maandishi. Hii ni haki ya msingi kwa kila utawala au uongozi.
Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe hakupewa mashtaka yake aliyakuta ndani ya kikao baada ya kupewa taarifa kwa ujumbe wa simu (text message au sms) ambapo kwa uzito wa makosa hayo yaliyosababisha kuvuliwa uongozi na kwa kuangalia athari zake kwake yeye binafsi na chama kwa ujumla, Kamati Kuu ilitakiwa kujiridhisha kwamba Kanuni za Uendeshaji na Katiba zinafuatwa.
Hili linaendana na utaratibu uliotumika kwa Samson Mwigamba kuvuliwa nyadhifa yake ya uenyekiti wa mkoa. Yeye hakuitwa kabisa kwenye kikao hicho na ni ukiukwaji wa Kanuni ya Uendeshaji
6.5.6(d) niliyoisoma hapo juu kwamba lazima kiongozi huyo aitwe kwenye kikao, sababu zilizotumika ingawaje hajapokea taarifa rasmi ya maandishi kwa mujibu wa Kanuni za Uendeshaji ni kwamba yeye ameshirki kwenye kuandaa na kusambaza waraka ambao unasemekana ni mkakati wa ushindi wenye lengo la kupindua uongozi uliopo.
Waraka huo haukumtaja Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe kama muandaaji au msambazaji. Waliouandaa hawajaukana na badala yake wamesema waziwazi kabisa kwa maneno na maandishi kwamba Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe HAHUSIKI. Sio sawa kumuadhibu Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe kwa hisia au tu kwa sababu ya urafiki wake na watu fulani.
Haya ni mapungufu ambayo kwa bahati nzuri Katiba na Kanuni za Uendeshaji zinatoa nafasi ya kurekebishwa kwa kutoa nafasi ya kukata rufaa. Na utaratibu ni huu hapa Kwa ufupi, Ibara 6.3.6(d) ya Katiba ya Chama kwamba “Kiongozi aliyechukuliwa hatua za kinidhamu na mamlaka yake ya nidhamu anayo haki ya kukata rufaa ngazi ya juu ya ile mamlaka yake ya nidhamu na uamuzi wa ngazi hiyo utakuwa wa mwisho”
Ibara 6.3.6(e) ya Katiba ya Chama “Rufaa yoyote lazima ifanyike katika muda wa siku thelathini tangu tarehe ya kupokea rasmi kwa maandishi maamuzi ya mamlaka iliyotoa adhabu”
Kanuni za Uendeshaji zinatoa UTARATIBU ambao unatakiwa ufuatwe ili kiongozi aliyeadhibiwa aweze kutumia HAKI yake ya kukata rufani kwa maneno haya, kanuni ya 6.5.8 ya Kanuni za Uendeshaji >> “Kiongozi aliyeadhibiwa atapewa taarifa ya msingi wa maamuzi ya mamlaka ya nidhamu ili kumuwezesha kuamua kukata rufani au la”
Kanuni ya 6.5.9 ya Kanuni za Uendeshaji >> “Mwadhibiwa atakayeamua kukata rufani atatakiwa kufanya hivyo katika muda wa siku thelathini baada ya kuarifiwa uamuzi wa adhabu”
Kanuni ya 6.5.10 ya Kanuni za Uendeshaji >> “Baada ya kutoa uamuzi kikao husika kinalazimika kuandaa
taarifa kamili ya mwenendo wa shauri na kuwasilisha ngazi ya juu. Taarifa hiyo lazima ifike katika muda wa siku kumi na nne baada ya kikao cha mamuzi”
Mpaka hivi sasa hatujapokea taarifa kamili ya mwenendo wa shauri tokea kikao cha Kamati Kuu cha tarehe 20-21/11/2013 Huo ndio utaratibu ambao Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe ameamua kufuata kwa kuheshimu maamuzi ya Kamati Kuu lakini kukatia rufaa maamuzi hayo. Kuheshimu maamuzi sio kuyakubali uhalali wake.
Kumekuwa na matukio ya kusikitisha ambayo mengine yamefikia mahali kuwa fujo na vurugu ikiwa ni pamoja na kurushiwa mawe Katibu Mkuu wa Chama ambapo baadhi ya vurugu hizo zimehusishwa na Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe na baadhi ya watu.
Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe hahusiki kwa njia yoyote na hayo yanayoendelea na anayakemea na kuwashauri wanachama wote kuwa watulivu na kuendelea kuwaheshimu viongozi wa kitaifa. Hatua zimeshachukuliwa kukata rufaa na ni imani yake kwamba Baraza Kuu la Chama litatenda haki kwa kupitia rufaa yake na kutoa uamuzi.

MILLARD AYO

Tusisubiri CNN Waiambie Dunia Mchango Wa Tanzania Kwa Ukombozi Wa Afrika.




Tusisubiri CNN Waiambie Dunia Mchango Wa Tanzania Kwa Ukombozi Wa Afrika...!

Kazi hiyo tuifanye sisi wenyewe.

nilimwona Rais wa
Ghana John Dramani Mahama akihojiwa na CNN kuhusiana na
Mandela. Mara tatu Rais huyo wa Ghana aliutaja mchango wa
Tanzania katika ukombozi wa Afrika ikiwemo Afrika Kusini ya Nelson
Mandela.
-Hivi ni wangapi wanajua kuwa kiongozi wa kwanza wa chama cha
ukombozi katika nchi huru ya Kiafrika ambaye Mandela alikutana nae
anaitwa John Mwakangale. Huyu alikuwa kiongozi katika TANU na
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
-Hivi ni wangapi wanajua kuwa Mji wa kwanza katika nchi huru ya
Kiafrika ambayo Mandela alikanyaga ardhi yake unaitwa Mbeya. Hivyo
basi, Tanganyika ndio nchi huru ya kwanza ya Kiafrika ambapo
Mandela alikanyaga ardhi yake.
- Hivi ni wangapi duniani wanajua, kuwa Julius Nyerere ndiye Rais wa
kwanza katika nchi huru ya Kiafrika ambaye Mandela alikutana nae. Na
ni Julius Nyerere baada ya kumkubali Mandela, ndiye aliyemsaidia
Mandela kwa kumtambulisha kwa Mfalme Haille Selassie wa Ethiopia?
Haikuwa ajabu, kuwa baada ya kutoka gerezani, kwa Mandela
Tanzania ikawa nchi ya kwanza kuitembelea.
Kumbukumbu hizi muhimu za kihistoria na nyinginezo Watanzania
hatupaswi kuisubiri CNN na vyombo vingine vya habari vya
kimagharibi viitangazie dunia.

Ni jukumu letu wenyewe.

Like · ·

Jumatatu, 9 Desemba 2013

Lwakatere Arudi tena Segerea

Wilfred Lwakatare · 1,293 followers
Yesterday at 1:03pm  ·
Habari Ya Asubuhi Waheshimiwa Marafiki,Ndugu na Jamaa,
Leo Mungu amenipa fursa ya kumtembelea Swahiba wangu Sheikh Issah Ponda gerezani Segerea pamoja na 'washkaji' wengine wengi niliojenga nao urafiki na undugu nilipokuwa gerezani.
Hivi sasa niko njiani kuelekea Segerea Gerezani.
Pamoja na kuwaona,nitawahabarisha yanayojiri mitaani,nitawapa moyo na kuwafariji na nimebebea 'mazagazaga' kibao.
Nawatakia siku njema.

Alicho Ongea zitto kabwe leo

KUTOKA KWA ZITTO KABWE LEO
"Matumaini yalikuwa makubwa sana mwaka 1961 Taifa letu lilipojikomboa kutoka makucha ya ukoloni. Vita 3 - Umasikini, Ujinga na Maradhi zilitangazwa. Azimio la Arusha likawa tumaini kubwa la kutokomeza umasikini, hasa wa vijijini.

Ni kweli tumepiga hatua kwenye Nyanja kadhaa. Ni dhahiri kuwa kwenye maeneo mengi tumerudi nyuma sana. Uwezo wetu wa kuzalisha Mali na kuondoa umasikini umepungua ambapo sasa uchumi unakua kwa wastani wa asilimia 7 lakini umasikini haupungui kwa sababu sekta ya wanyonge-kilimo, imedumaa. Takribani mazao yetu yote ya kilimo tunauza nje kama ghafi tofauti na miaka ya 1970 ambapo tulianza kuongeza thamani kama Korosho, Kahawa, Pamba na Katani. Tumerudishwa nyuma na ubinafsishaji na menejimenti za hovyo hovyo.

Elimu sasa ni bora elimu na sio elimu bora maana watoto hawajifunzi mashuleni na hata wahitimu wa vyuo vikuu uwezo wao kukabili changamoto za nchi makazini ni mdogo sana.

Afya ya wananchi bado mbaya kutokana na wananchi wengi kufariki kwa magonjwa yanayotibika.

Miaka 52 baada ya Uhuru ni asilimia 6 ya Watanzania wana hifadhi ya jamii. Wakulima wetu bado hawana bima ya mazao yao wala pensheni.
Changamoto ya kizazi cha sasa cha viongozi ni ku transform nchi ili kuongeza uwezo wa uzalishaji, kuongeza ajira, kupunguza inequality na kujenga Taifa imara mbele ya mataifa"

Jumapili, 8 Desemba 2013

Ukistaajabu ya Zitto utayaona ya Lowasa

Lowassa Ngoyai Edward Kaingia Choo cha Kike baada ya kwenda Nigeria akaambiwa na Mtumishi maarufu wa mungu nabiiTB Joshua kwamba mh.Lowassa ndiye rais ajaye wa Tanzania,
Kwasasa katika Africa watu wanatia mashaka makubwa ya Utabili wake kwani kila ambacho anasema kinakuwa tofauti baada ya kutabili kuwa Kuna Raisi wa East Africa atatekwa na Al-Shabab na amna kilichoweza kutokea na aliweza kutabili mambo mbalimbali kwasasa nchini nigeria yanaenda tofauti,
Na Lowassa kaingia katika Choo cha kike baada ya kuambia agawe pesa tu katika majumba ya ibada atapata Urais kumbe utabili ni feki baada ya kuona kuwa Lowassa kwasasa anapingwa sana ndani ya chama chake na mpaka upinzani kwa hasara ambayo ameingizia taifa letu na kamwe amwezi pata urais ndoto za alinacha,

TBjoshua amekuwa msanii kuwalia pesa mafisadi wakubwa Duniani. — in Kibondo, Kigoma, Tanzania.
Like ·

Jumamosi, 7 Desemba 2013

Haya ndo madhara ya Kugundulika kwa Dawa ya Ukimwi


Ikiwa ni siku kadhaa zimekatika tangu kutolewa kwa taarifa ya kupatikana kwa tiba ya Ukimwi, vitendo vya ufuska katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam vimeonekana kuongezeka kwa kasi ya ajabu huku joto lake likikadiriwa kufikia nyuzi joto 90, Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili.

Uchunguzi uliofanywa mara baada ya kutolewa habari hiyo umebaini kuwa, baadhi ya watu hasa machangudoa wameongeza spidi ya kufanya ngono zembe na wengine kudiriki kusherehekea kufanya hivyo.

Imebainika kuwa kupatikana kwa dawa hiyo kumewafanya hata wale waliokuwa wakiogopa kufa kwa kuhakikisha wanafanya ngono salama, kuingia kwenye hatari hiyo kwa kasi mpya, wakiamini kuwa hata wakiukwaa Ukimwi dawa ipo.

Katika sehemu ya uchunguzi huo,maeneo mbalimbali ya jiji yanayosifika kwa biashara ya uchangudoa na kushuhudia shamra shamra za aina yake zilizohusishwa na upatikanaji wa tiba hiyo ya ngoma.

Miongoni mwa maeneo hayo ni Kinondoni, Oysterbay karibu na Oysterbay Hotel, Manzese Uwanja wa Fisi, Jolly Club na Buguruni ambapo dadapoa hao walionekana kuwa na nyuso za furaha huku baadhi wakipaza sauti kwa kusema: “Dawa ya Ukimwi imepatikana sasa ni kujiuza kwa kwenda mbele na hakuna kutumia kondomu.”

Eneo la Afrika Sana, Sinza, baadhi ya dada poa walioelezwa uwepo wa mkono wa sheria hata kama tiba ya Ukimwi inaelezwa kupatikana, walijibu: “Sheria nsheria nini? Huyo Kova atukome kwanza, kwa sababu kama dawa ya Ukimwi imepatikana tatizo lingine la nini? Atupe uhuru jamani!” 

Katika hali ya kustaajabisha katika eneo la Kinondoni Makaburini, baadhi ya machangudoa walifanya pati ya kusherehekea ujio wa dawa hiyo kwa kunywa pombe na kula nyama choma.

Wakiongea na  katika nyakati tofauti wauza miili hao walisema kuwa, ujio wa dawa hiyo ni mkombozi kwao kwani itawaweka katika nafasi nzuri ya kufanya biashara hiyo kwa kujiachia zaidi tofauti na ilivyokuwa huko nyuma.

Walisema, awali walikuwa wakilazimika kukaribisha majadiliano kati yao na wateja wao kuhusiana na kutumia au kutotumia kondomu ambapo bei zilikuwa zikitofautiana lakini sasa bei itakuwa ni moja tu.

“Kwa kweli taarifa za kupatikana kwa dawa hii tumezipokea kwa furaha sana, hii itatufanya tuwe huru kufanya biashara hii tofauti na huko nyuma ambapo tulikuwa tukitumia kondomu kwa shingo upande, sasa ni full kujiachia,” alisema dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mwanaidi White mkazi wa Buguruni ambaye hufanya biashara hiyo eneo la Kinondoni.

Uchunguzi huo pia imebainika kuwa soko la kondom sasa limeshuka kwa kiasi kikubwa kwani licha ya machangudoa hata baadhi ya wapenzi, wemeanza kutoona sababu ya kutumia kifaa hicho ambacho bado kina umuhimu mkubwa katika kujikinga na VVU.

Katika uchunguzi huo pia, imebainika kuwepo kwa  baadhi ya SMS ambazo baadhi ya watu wanatumiana na nyingine katika mitandao ya intaneti kama barua pepe na facebook.
Ujumbe huo, una maudhui ya kuwataka watu kutojali chochote kwa sababu dawa ya Ukimwi imepatikana.

“Ni zamu yetu kutesa wadau. Ukimwi umesumbua mno akili yetu. Sasa dawa imepatikana, kondomu zinaenda likizo mpaka uje ugonjwa mwingine,” unasomeka ujumbe huo ambao unasambazwa kwa SMS na barua pepe na facebook.

Hata hivyo, wananchi wantahadharishwa kuwa, upatikanaji wa dawa hiyo isiwe sababu ya kujiachia na kujiweka katika mazingira ya kupata maambukizi kwani Ukimwi bado ni ugonjwa hatari.

Inashauriwa watu kuendelea kujali afya zao kwani umakini usipokuwepo, vifo vingi vinaweza kutokea hasa itakapotokea dawa hiyo kuchelewa nchini. Aidha, hata bila Ukimwi, kondomu ni muhimu kwa ajili ya magonjwa mbalimbali ya zinaa.
GPL