Alhamisi, 16 Januari 2014

Pinda atatua Mapigano ya wakulima na Wafugaji mkoani Manyara









Waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania mheshimiwa Mizengo Pinda Leo katika wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara amezungumza na wakulima pamoja na wafugaji waliokuwa wakipigana kwaajili ya maeneno ambayo Serikali inadai kuwa ni hifadhi ya wanyama na mali asili
 Wafugaji wenye asili ya kimasai wao wanawafukuza wakulima kwamadai kuwa wakulima wanaharibu mazingira na ndomana serikali inawataka wote watoke katika hifadhi hiyo,  pia na wao wao wanakosa maeneo ya malisho kwaajili ya mifugo yao.
 Leo akiongea na Wakulima pamoja na Wafugaji hao Waziri mkuu ametaka hekima na utaratibu mzuri ufuatwe katika kuwahamishwaji wa wakulima na wafugaji. Pia akaeleza kuwa kama eneo hilo ni hifadhi na vijiji vyote vinavyo zunguka eneo hilo viliridhia basi si mfugaji wala mkulima mwenye haki ya kufanya shughuli  yoyote ile katika eneo hilo. Lakini kama vijiji havikuridhia katika uhamishaji wa eneo hilo na kulifanya kuwa hifadhi Basi wakae wajadili kwa pamoja na eneo hilo lirudishwe mikononi mwa wana vijiji hao.
Hadi mwisho wa mkutano huo hakuruhusu wakulima   kuendelea kulima wala wafugaji kuendelea kufuga katika maeneo hayo na kuona kama wao ndo wanao stahili kuwepo hapo. Nakutaka mapigano yasiwepo tena
Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Afrika.

Hakuna maoni: