Jumatatu, 3 Machi 2014

WIZARA YA ELIMU ELIMU TANZANIA YAZIDI KUBORONGA



                                                   
    Wizara ya elimu ya Tanzania imeendelea kufanya hovyo katika maamuzi na utendaji wa           mambo   yake.
 Halii hii inajidhihirisha kwa kuwapa walimu tarajali (walimu waliopo vyuo vya Serikali,wa ngazi ya cheti na Stashahada) pesa  ya kujikimu  wakiwa  katika mazoezi ya vitendo  (field) kiasi cha  shilingi  4500 (elfu mianne na miatano tu ) .
Hii sio bahati mbaya kwa sababu utaratibu huo wakuwapa wanavyuo hao wanaosomea ualimu ulianza mwaka jana na walilipwa pia 4500 wakiwaahidi kuwa kwa  kuwa ni mfumo mpya hivyo mwaka utakaofuatia yaani mwaka huu wa 2014 wange waongeza pesa lakini hali imebakia kuwa hivyo hivyo.

Utaratimu wa miaka yanyuma 2012 kurudi nyuma ilikuwa wanachuo walio katika vyuo vya ualimu vya serikali  wanapoenda kwenye mazoezi ya vitendo walikuwa wakipewa chakula na fedha kiasi za kujikimu wanapo kuwa huko lakini kwanzia mwaka jana wamekuwa wakipewa shilingi 4500 tu.
 Katika hali ya kawaida tujiulize hiyo pesa inatosha nini ikiwa wanavyuo waliopo vyuo vikuu huwa wanalipwa shilingi 7500 kwa siku kama pesa yao ya kula wakiwa chuoni na wanapo enda (field) kwenye mazoezi ya vitendo huwa walipwa (10000) elfu kumi .

 Ukiangalia mazingira ya hawa walimu wavyuo vikuu na wa stashahada hata Cheti  wote wanaenda Field maeneo yale yale na maanisha shule zile zile na kama changamoto ni sawa tu sasa kwanini kuwe na tofauti  za posho za kujikimu wanapo kuwa huko huu ni udhaifu wa hali ya juu Wizara inabidi iji sahihishe katika upangaji wake wa mambo.Na hiyo pesa ya shilingi 4500 haitoshi kwa maisha ya sasa mtasababisha wadogo zetu wakike kujiuza huko na kuvunja ndoa za watu.
Kama haiwezekani utaratibu wa zamani ukirudishwa ni vizuri pia.

Maana ikiwa watu wanagomea laki tatu Bungeni kwenye Bunge La katitiba  hawa wanaokubali 4500 unadhani vichwani mwao wafikiria nini  kama sio ni mgomo baridi?.
   
Nchi yenye utawala Bora haiwezi kuwandaa Bora walimu na sio Walimu Bora.
                              Wakikuuliza kaandaa nani waambie korumba Mtanzania

Hakuna maoni: