Ijumaa, 6 Desemba 2013

Chadema UDOM Watoa Tangazo ni juu ya kuvuliwa uongozi kwa Zitto

CHADEMA NDANI YA UDOM.
Sisi wanaharakati tulioko Udom,kesho tutafanya mkutano pale nje kidogo ya kitivo cha Elimu, lengo ni kuwaelimisha vijana wenye mawazo ya ki-CCM, hapo tutaonesha jinsi chadema ilivyo imara na ilivyo na uwezo wa kuchukua maamuzi magumu ndani ya chama kwa maslahi ya taifa kitu ambacho ccm hawawezi kwani walisha shindwa, mfano ni pale CCM iliposhindwa kuwavua gamba magamba wao kwa sababu ndani ya ccm hakuna msafi awezaye kumnyooshea mwenzake kidole-wote ni mafisadi tofauti na CHADEMA ambayo kila mmoja ni msafi kwa nafasi yake na akijitokeza msaliti,dhaifu, na fisadi anaondolewa haraka na kimbilio huo ni CCM kwani ndicho kichaka cha waovu,chadema hatuna nafasi ya waovu.nitumie nafasi hii kuwaalika kwenye mkutano huo wa kesho jumamosi pale UDOM kwenye ofisi zetu, mliopo udom na nje ya UDOM tunaomba mtuunge mkono, muda si mrefu tutaanza kutoa elimu kuhusu katiba ya chadema na nchi kupitia blog yetu ambayo ntaitangaza kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo kundi hili, lengo ni kuwaelimisha watanzania kuongea kwa kutumia mareje ya vifungu vya sheria kwa sababu haki hapelekewi mtu bali huidai mwenyewe.kwa maana hii basi bila kuifahamu sheria inayokupa haki fulani huwezi kuidai haki, hii ndo nafasi ambayo mafisadi wanaitumia kutunyang'anya haki yetu watanzania. Watanzania simameni tudai haki zetu, na CHADEMA ndilo jiko la walio bobea sheria, ukiwa mwana-chadema tayari wewe ni mwanasheria kwa maana moja ya jukumu letu ni kuielimisha jamii kuhusu utawala wa kisheria. Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki CHADEMA, Mungu ibariki CHADEMA tawi la UDOM. Katibu wa CDM-Tawi la UDOM. Marigiri.

Hakuna maoni: